ELCT North Eastern Diocese
Ibada ya Jumapili KKKT-DKMs Usharika wa Duga
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu leo tarehe 09/01/2022 ameongoza Ibada ya jumapili katika Usharika wa Duga Jimbo la Pwani.awali Baba Askofu aliweka jiwe la msingi katika nyumba ya mtumishi.Liturgia katika Ibada hiyo iliongozwa na mkuu wa Jimbo la Pwani Mch.Thadeus A. Ketto.


Ibada ilihudhuriwa na Wachungaji, Wainjilisti,Mashemasi,Kwaya,Washarika pamoja na watu mbalimbali kutoka ndani na nje ya Usharika wa Duga.




- Hits: 14722
Ibada ya Jumapili Usharika wa Mbaramo Mtaa wa Mlesa
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt.Msafiri Joseph Mbilu leo tarehe 02/01/2022 ameongoza Ibada ya Jumapili katika Usharika wa Mbaramo Mtaa wa Mlesa, Imekuwa siku ya Baraka tele kwa washarika wa Usharika wa Mbaramo mtaa wa Mlesa. Ibada hiyo ilikuwa na matukio mbalimbali ikiwemo uwekwaji wa jiwe la msingi katika nyumba ya mtumishi pamoja na kufunguliwa kwa mnara wa kengele.
- Hits: 14404
Ibada ya mwaka mpya 2022 Usharika wa Vuga
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ametoa wito kwa watunzi wa nyimbo,mashairi, na sanaa mbalimbali kuendelea kutumia neno Kuu la Dayosisi linalo toka katika kitabu cha Zaburi ya 32:8 katika utunzi wao.
Wito huo ameutoa leo tarehe 01/01/2022 kwenye Ibada ya mwaka mpya iliyofanyika katika Usharika wa Vuga jimbo la Kusini.Baba Askofu Mbilu amesema kuwa bado ipo sababu ya kuendelea kufundishwa na kuoneshwa njia katika utumishi na hivyo neno kuu la mwaka jana litaendelea kutumika katika mwaka huu.

Kwa upande mwingine Halmashauri Kuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki imeona ni vema mwaka huu wa 2022 uwe mwaka wa wanawake kwani wanawake ni jeshi kubwa na imara hivyo wanao uwezo wa kuweka mipango mbalimbali na endelevu ili kuiinua na kuijenga Dayosisi.
Wito unaletwa kwa wanawake wote wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kuupokea mwaka huu kuanzia kwenye ngazi za Mitaa, Sharika, Majimbo hadi ngazi ya Dayosisi.ni matumaini ya uongozi wanawake wataweka mipango mbalimbali ili kuenzi mwaka huu.

- Hits: 14883
Page 92 of 137



