ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • Askofu Dkt. Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Helga Walter

    Askofu Dkt. Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Helga Walter

    Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Mbilu, alipata fursa ya kupokea ugeni w...
  • Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu KKKT-DKMs

    Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu KKKT-DKMs

    Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania – Dayosi...
  • Askofu Dkt. Mbilu aweka wakfu pikipiki rasmi kutumika Idara ya Mashamba

    Askofu Dkt. Mbilu aweka wakfu pikipiki rasmi kutumika Idara ya Mashamba

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Jos...
  • Askofu Dkt. Mbilu Aongoza Kikao Kazi cha Wachungaji

    Askofu Dkt. Mbilu Aongoza Kikao Kazi cha Wachungaji

    Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameongoza kikao kazi cha W...
  • TUZO YA PONGEZI KWA KUCHANGIA DENI LA DAYOSISI

    TUZO YA PONGEZI KWA KUCHANGIA DENI LA DAYOSISI

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

Askofu Dkt. Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Helga Walter

  • Print
Details
Published: 05 February 2026

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Mbilu, alipata fursa ya kupokea ugeni wa kiongozi wa undugu Helga Walter kutoka Hainberg-Gymnasium Göttingen  nchini Ujerumani. 

Katika mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki tarehe 05/02/2026  , pande zote mbili zilijadili kwa kina namna ya kuendelea kuimarisha na kuboresha undugu uliopo kati yao, hususani katika nyanja za elimu na huduma za kijamii.

Aidha, Askofu Dkt. Mbilu alitumia fursa hiyo kutoa shukrani za dhati kwa Helga pamoja na wadau wengine wa maendeleo kutoka Hainberg-Gymnasium Göttingen kwa michango yao ya kimaendeleo, hususani katika Shule ya Sekondari Lwandai pamoja na vituo vya diakonia vilivyopo Irente vinavyomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.

Ziara hiyo ilionesha mshikamano na dhamira ya pamoja ya kuendeleza ushirikiano wenye tija kwa manufaa ya jamii.

Hits: 88

Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu KKKT-DKMs

  • Print
Details
Published: 29 January 2026

 

Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) kilichofanyika  tarehe 29 Januari 2026 katika Ukumbi Mdogo wa Mikutano, Utondolo – Lushoto. Kikao hicho kimewakutanisha wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa ajili ya kujadili na kufanya maamuzi muhimu yanayohusu uendeshaji na maendeleo ya dayosisi.

Hits: 827

Askofu Dkt. Mbilu aweka wakfu pikipiki rasmi kutumika Idara ya Mashamba

  • Print
Details
Published: 28 January 2026

 

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameongoza Ibada ya kuweka  wakfu chombo cha usafiri (pikipiki) na kumkabidhi kadi ya pikipiki pamoja na ufunguo Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uchumi, Mipango na Maendeleo, Bi. Pendo Lauwo, kwa ajili ya shughuli za kikazi za kila siku za Idara ya Mashamba.

Ibada hiyo pamoja na makabidhiano hayo yamefanyika tarehe 28/01/2025 katika Ofisi za Makao Makuu ya Dayosisi, Lushoto-Tanga. Chombo hiki cha usafiri kitasaidia katika mazingira ambayo hakuna barabara zinazofikika kwa kutumia usafiri wa gari.

Hits: 825

Read more ...

Askofu Dkt. Mbilu Aongoza Kikao Kazi cha Wachungaji

  • Print
Details
Published: 13 January 2026

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ameongoza kikao kazi cha Wachungaji kilicholenga kuweka mipango yamwaka 2026 na kufanya tathmini ya hali ya Deni la Dayosisi pamoja na kuweka mikakati mipya ya pamoja ya kulikabili na kulimaliza.

Kikao hicho kimefanyika tarehe 13 Januari, 2026 katika Usharika wa Kanisa Kuu Lushoto, kikihusisha Wachungaji kutoka sharika mbalimbali za Dayosisi. Lengo kuu la kikao kilikuwa ni kuimarisha ushirikiano, kuweka mikakati shirikishi,kupanga na kuendeleza mipango ya utekelezaji kwa mwaka 2026, ikiwemo mpango mahsusi wa kumaliza deni la Dayosisi.

Akifungua kikao hicho, Askofu Dkt. Mbilu aliwashukuru kwa dhati Wachungaji, watumishi na Washarika wote wa Dayosisi kwa moyo wa kujitoa na ushiriki wao mkubwa katika kuitenda kazi ya Bwana, hususani katika kuchangia deni la Dayosisi. Alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwa waaminifu, na watu wenye mshikamano na  maono ya pamoja kwa maendeleo ya Kanisa.

 Katika kikao hicho pia kulifanyika zoezi la utoaji wa tuzo ya pongezi kwa moja ya usharika uliofanya vizuri katika uchangiaji wa deni la Dayosisi. Uongozi wa Dayosisi ulimpongeza kwa kipekee Mch. Anna Msisili wa Usharika wa Ubiri pamoja na washarika wa Usharika huo, ambao wamefanikiwa kukamilisha kiwango chote cha uchangiaji wa deni la Dayosisi na kushika nafasi ya KWANZA kati ya sharika 76 za Dayosisi kwa kutimiza lengo kwa wakati.Zoezi hili lilifanyika katika sehemu ya ufunguzi wa kikao hicho.

Tuzo hiyo ilipokelewa na Mchungaji  Anna Msisili, aliyeambatana na Wazee wa Kanisa wa Usharika huo.Tuzo hiyo ni miongoni mwa tuzo zinazotolewa kwa sharika 10 za mwanzo zitakazokamilisha deni kwa wakati, na inabeba ujumbe wa neno la Mungu kutoka Kutoka 33:14 unaosema: “Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.”

Aidha, taarifa ya kina kuhusu hali ya uchangiaji wa deni la Dayosisi kwa kila usharika iliwasilishwa kwa Wachungaji na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Dayosisi, CPA Peter John Singano. Ilielezwa kuwa taarifa rasmi kwa Washarika wote itatolewa tarehe 18 Januari, 2026, na itasomwa katika sharika.

Hits: 1471
  1. TUZO YA PONGEZI KWA KUCHANGIA DENI LA DAYOSISI
  2. Heri ya Mwaka Mpya 2026
  3. Askofu Dkt. Mbilu Akabidhi Gari 1 kwa Kituo Cha Lutindi Mental Hospital
  4. ELCT-NED FAMILY BONANZA 2025

Page 1 of 135

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • ...
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese