ELCT North Eastern Diocese
Tamati ya juma la vijana Kanisa Kuu Lushoto
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt Msafiri Joseph Mbilu amewapongeza vijana wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kipekee vijana wa Kanisa Kuu Lushoto kwa kazi kubwa na nzuri waliyo ifanya kwa njia ya nyimbo na walio ongoza Ibada
pongezi hizo amezitoa leo tarehe 20/02/2022 kwenye Ibada ya sikukuu ya Vijana huku akimpongeza mratibu wa Vijana na ukwata wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Alice Kopwe kwa maandalizi mazuri yanayoondelea kuelekea tamasha la Vijana na Askofu litakalo fanyika tarehe 25-27/02/2022.
- Hits: 14959
Mkuu wa Wilaya ya Lushoto atoa wito kwa viongozi wa dini
- Details

Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Mhe. Kalisti Lazaro ametoa wito kwa kamati ya amani ya viongozi wa Dini mbalimbali (Interfaith) kuendelea kuwa mabalozi wa kulinda amani na upendo kwa kuhubiri katika nyumba zao za Ibada ili kuzuia matukio ya ukatili pamoja na mauwaji ambayo yamekuwa yakishamiri maeneo mbalimba Nchini sambamba na kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa sensa ambayo inatarajiwa kufanyika mwezi wa nane mwaka huu.
- Hits: 16788
Ibada ya kuingizwa kazini,Katibu Mkuu,Mkurugenzi wa fedha pamoja na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt Msafiri Joseph Mbilu ameongoza Ibada ya kuingizwa kazini kwa Katibu Mkuu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Godfrey Tahona Walalaze, Mkurugenzi wa fedha na utawala CPA Peter John Singano pamoja na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya KKKT-DKMs, leo tarehe 06/02/2022 katika Usharika wa Korogwe.Katika kikao cha Halmashauri Kuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki iliyoketi Utondolo Lushoto tarehe 9-10/12/2021 ilimthibitisha Mch. Godfrey Walalaze Kuwa Katibu Mkuu na CPA Peter John Singano kuwa Mkurugenzi wa fedha na Utawala.
- Hits: 15606
Semina elekezi
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu leo tarehe 05/02/2022 ameongoza semina elekezi kuelekea siku ya kuingizwa kazini kwa Katibu Mkuu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Godfrey Tahona Walalaze,Mkurugenzi wa fedha na Utawala wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, CPA Peter John Singano pamoja na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki hapo kesho tarehe 06/02/2022.
- Hits: 14164
Page 89 of 137

