ELCT North Eastern Diocese
Wana KKKT-DKMs kazini kukabiliana na deni la Dayosisi.
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amechukuwa hatua ya kuwaandikia barua washarika waliopo ndani ya Dayosisi juu ya ombi la mchango kwaajili ya kukabiliana na deni la Dayosisi.
Akizungumza leo tarehe 10/04/2022 katika Ibada ya Jumapili iliyo ambatana na uzinduzi wa uchangiaji wa deni hilo katika Usharika wa Kana Tanga, amewashukuru wana Dayosisi kwa jinsi wanavyojitoa katika kumtumikia Mungu na kujitoa kwao kwa hali na mali katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili Dayosisi.

Mkuu wa Jimbo la Pwani, Mch. Thadeus A. Ketto
Askofu Dkt. Mbilu anachukua hatua hii kutokana na Dayosisi kudaiwa madeni makubwa na miongoni mwa madeni hayo ni hatarishi sana kwani yanaweza kusababisha mali za Dayosisi mfano Majengo, Mashamba, Magari nk. kupigwa mnada ili kufidia gharama za wale wanaoidai Dayosisi. Ofisi ya Katibu Mkuu imeanza kupokea taarifa za awali juu ya hatua hizo juu ya mali za Dayosisi kupigwa mnada.

Mkurugenzi wa fedha na Utawala KKKT-DKMs CPA. PETER JOHN SINGANI
Kwa ujumla deni la Dayosisi lililorithiwa toka Uongozi uliopita ni takribani Tsh. 7,000,000,000 (Bilioni Saba) likiwepo deni la mkopo wa CRDB, Mishahara na stahiki za watumishi wengine katika vituo mbalimbali vya Dayosisi kama vile Ofisi Kuu, SEKOMU, pamoja na madeni ya Mifuko ya kijamii kama vile NSSF, PSSSF pamoja na kodi mbalimbali.

Kwa kupitia sadaka ya maendeleo ya KKKT-DKMs imeendelea kupunguza baadhi ya madeni hayo kama vile deni la CRDB na sasa limeshuka kutoka Tsh. 1,200,000,000 (Bilioni Moja na nukta 2) hadi kufika Tsh.792,000,000 (Milioni Mia saba na Tisini na Mbili). Na hapa Askofu Dkt. Mbilu anamshukuru Mkuu wa Jimbo la Pwani Mch. Thadeus A. Ketto, Washarika wa Kana na wana Dayosisi kwa ujumla kwa jinsi wanavyoendelea kujitoa katika utoaji wa sadaka hiyo.

Hata hivyo ili kuweza kukabiliana na madeni hayo makubwa, Askofu Dkt. Mbilu analeta ombi kwa washarika kwani wao ni kiungo muhimu cha Dayosisi hii kuchangia deni hilo kama viwango vilivyo ainishwa kwenye barua walizo pokea kwa kadri Bwana atakavyowajalia. Na hapa anawaomba wana Dayosisi katika awamu hii ya kwanza kuanza kuchangia sehemu ya deni hilo katika kipindi cha miezi sita yaani kuanzia tarehe 01/04 hadi tarehe 31/10/ 2022.

Ili kuweza kuhakikisha kuwa fedha hizi zinafika mahali sahihi, kwa wana Dayosisi waliopo ndani ya Dayosisi wanaombwa kuingiza fedha hizo moja kwa moja kwenye akaunti ya Dayosisi ambayo ni: -
- NMB HARAMBEE ACCOUNT No. 41610027028 au
- CRDB ELCT NORTH EASTERN DIOCESE Acc.No.01J1029661501

Askofu Dkt. Mbilu ametanabaisha kuwa hatua ya pili ya uchangiaji kwa wadau wa maendeleo na wana KKKT-DKMs waliopo nje ya Dayosisi utatangazwa hivi karibuni. Uongozi unakutakia baraka za Mungu katika Utumishi wako shambani mwa Bwana.


- Hits: 15547
Askofu Dkt. Msafiri Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF).
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF) Mch. Anne Burghardt katika Ofisi za Makao Makuu ya KKKT (Arusha) ambapo Katibu Mkuu huyo yupo Nchini Tanzania kwa ziara ya Kikazi katika Kanisa la KKKT.
Aidha, Askofu Dkt. Mbilu ni mmoja kati ya wanakamati ya Ibada na Muziki ya Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF) inayoandaa Mkutano Mkuu utakaofanyika Nchini Poland mwakani
Kamati hii iliundwa mwaka 2021 na ofisi ya Katibu Mkuu wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani ambayo makao Makuu yake yapo Geneva Uswis. Kamati hii ina wajumbe kumi kutoka Ujerumani,Canada,Norway,Hungary,Poland,Hong Kong,USA,Brazil,Switzeland na Africa ambapo mjumbe muwakilishi ni Askofu Dkt. Msafiri Mbilu.

- Hits: 13504
Kikao cha Halmashauri ya Mipango na fedha
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mchungaji Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameisihi Halmashauri ya Mipango na fedha kuketi na kupitia mpango mkakakati wa Dayosisi kwa umakini mkubwa kuchambua na kutoa maoni yenye tija ili utekelezaji wake uweze kuja kuwa na tija.

Askofu Dkt Mbilu ametoa rai hiyo leo tarehe: 22/03/2022 wakati akifungua kikao cha Halmashauri hiyo ya Mipango na fedha ya Dayosisi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Utondolo Wilayani Lushoto.

Halmashauri hiyo inajadili na kupitisha mpango mkakati wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, ili upelekwe kwenye Halmashauri Kuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ili kuujadili na kuupitisha rasmi mpango mkakati wa Dayosisi na baaadae uweze kutumika katika Dayosisi nzima. Mpango Mkakati huo ni wa kipindi cha miaka 5 kuanzia 2022 hadi 2026.

Katika ufunguzi Askofu Dkt Mbilu alihubiri neno la Mungu kutoka kitabu cha Injili ya Luka 14:28, na kuongeza kuwa ni imani yake utendaji kazi wao utampa Mungu Utukufu kwani mpango huo utakuwa ni Dira ya Dayosisi.

- Hits: 13599
Tangazo la zabuni ya ununuzi wa madini ya dhahabu – Bangala
- Details

TANGAZO LA ZABUNI YA UNUNUZI WA MADINI YA DHAHABU – BANGALA
Katibu Mkuu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, anapenda kuwatangazia wazabuni na makampuni yenye sifa ndani na nje ya Wilaya ya Lushoto kwamba yanakaribishwa kutuma maombi ya zabuni ya kununua madini aina ya Dhahabu katika kata ya Vuga Kijiji cha Kihitu- Bangala (Eneo linalo milikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki).Mwombaji aambatanishe kivuli cha leseni hai ya biashara na hati ya usajili ya mlipa kodi (TIN) na aoneshe eneo lake la biashara (Physical Address).Utaratibu wa kutuma maombi, tuma maombi katika bahasha na isioneshe alama yoyote ya utambulisho wa mwombaji. Ada ya maombi ni Tsh. 30,000 itumwe kwenye akaunti namba 41606600224 NED-ELCT MFUKO WA FAIDA.Tuma maombi yako kwa,Katibu Mkuu KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,S.L.P 10 Lushoto,Maombi yatumwe kabla ya tarehe 25/03/2022

- Hits: 14232
Page 86 of 137

