ELCT North Eastern Diocese
LUSHOTO ILIVYO SIMAMA KUSHUHUDIA ASKOFU DKT. MSAFIRI MBILU AKIINGIZWA KAZINI
- Details

JUMAPILI ya Mei 9 mwaka 2021, shughuli za mji wa Lushoto na viunga vyake zilisimama kwa muda huku macho na masikio yote yakiwa kwenye tukio la Ibada ya kuingizwa kazini kwa Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu kuwa Askofu wa awamu ya tano wa KKKT-DKMs.
Leo tarehe 09/05/2022 Askofu Dkt Msafiri Mbilu anafikisha mwaka mmoja tangu kuwekwa wakfu kuwa Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.Askofu Dkt Mbilu anaendelea kuwakumbusha watumishi kusimama imara ili kuhubiri neno la Mungu kwa usahihi na kusimamia mafundisho sahihi ya neno la Mungu na kuondokana na mafundisho potofu yanayopelekea kujenga roho ya uvivu na wasiwasi katika jamii.

Mhadhiri huyo mwandamizi wa chuo Kikuu cha Silliman cha Nchini Ufilipino, aliingizwa kazini katika Ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Lushoto na kisha yeye kumuingiza kazini Msaidizi wake, Mch. Michael Mlondakweli Kanju.
ILIVYOKUWA
Ibada ilianza kwa maandamano kutoka yalipo Makao Makuu ya Dayosisi hiyo, yaliyopo katikati ya Mji wa Lushoto na kuelekea Kanisa Kuu huku waki jipanga kwa kuongozwa na mbeba msalaba,

wabeba bendera ya Dayosisi na wapiga tarumbeta ambao walikuwa zaidi ya mia moja.Wapiga tarumbeta walikuwa kivutio kikubwa kwani walikuwa mahiri katika upigaji wao, pia walikuwa na sare ya pamoja ya mashati meupe na suruali nyeusi kwa wanaume na wanawake sketi nyeusi.
- Hits: 15031
Taarifa ya mchango wa kukabiliana na deni la Dayosisi kwa mwezi April
- Details

Uongozi wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kupitia kwa Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu umeanza utekelezaji wa ahadi waliyoitoa juu ya utaoji wa taarifa ya fedha zinazochangwa na Wanadayosisi zitakazo saidia kukabiliana na Deni la Dayosisi.
Ikumbukwe kua mnamo tarehe 24/03/2022 Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu aliwaandikia barua wana Dayosisi kuwaomba kuingia kazini ili kukabiliana na madeni makubwa yanayoikabili Dayosisi ambayo kwa ujumla wake ni hatarishi kwani yanaweza kusababisha mali za Dayosisi kupigwa mnada, kudumaza Dayosisi kwa muda mrefu, kutokuaminiwa na wadau wa maendeleo, kuathirika kwa Misioni pamoja na kufisha maono ya viongozi.
- Hits: 14269
Uchimbaji wa madini waanza Vuga Kihitu
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amezindua rasmi shughuli za uchimbaji wa madini Vuga Kihitu yaliyopo katika shule ya sekondari ya Bangala na kuwataka wachimbaji kufuata na kuheshimu sheria zilizowekwa ili kulinda na kudumisha amani.

Akimuwakilisha Askofu Dkt. Mbilu katika uzinduzi huo msaidizi wa Askofu Mch. Michael Kanju amesema kuwa uchimbaji huo unafanyika kwa mujibu wa sheria za Nchi hivyo kuwataka wachimbaji hao kutokuvunja sheria sambamba na kuwaasa kutambua eneo hilo ni sehemu ya kuwainua kiuchumi.
- Hits: 14875
Ibada ya kuingizwa kazini kwa msaidizi wa Askofu KKKT-Dayosisi ya Mkoani Mara
- Details
SEHEMU YA MATUKIO KATIKA PICHA, Ibada ya kuingizwa kazini kwa msaidizi wa Askofu KKKT-Dayosisi ya Mkoani Mara. Mch Eliya Kisarema Bwigeki iliyofanyika tarehe 24/04/2022, Msaidizi wa Askofu KKKT-DKMs, Mch Michael Mlondakweli Kanju alimuwakilisha Askofu wa KKKT-DKMs Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu katika Ibada hiyo.

- Hits: 16736
Page 84 of 137

