ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI YA KAZI Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya...
  • Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji  NSSF

    Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF

    Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifa...
  • TAARIFA

    TAARIFA

    Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, u...
  • ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Jos...
  • Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Dayosisi yetu imepata heshima kubwa ya kushiriki katika Mkutano wa Kanda ya Afrika ulioandaliwa na U...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

LUSHOTO ILIVYO SIMAMA KUSHUHUDIA ASKOFU DKT. MSAFIRI MBILU AKIINGIZWA KAZINI

  • Print
Details
Published: 09 May 2022

 

JUMAPILI ya Mei 9 mwaka 2021, shughuli za mji wa Lushoto na viunga vyake zilisimama kwa muda huku macho na masikio yote yakiwa kwenye tukio la Ibada ya kuingizwa kazini  kwa Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki  Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu kuwa Askofu wa awamu ya tano wa KKKT-DKMs.

Leo tarehe 09/05/2022 Askofu Dkt Msafiri Mbilu anafikisha mwaka mmoja tangu kuwekwa wakfu kuwa Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.Askofu Dkt  Mbilu anaendelea kuwakumbusha watumishi kusimama imara ili kuhubiri neno la Mungu kwa usahihi na kusimamia mafundisho sahihi ya neno la Mungu na kuondokana na mafundisho potofu yanayopelekea kujenga roho ya uvivu na wasiwasi katika jamii.

 Mhadhiri huyo mwandamizi wa chuo Kikuu cha Silliman cha Nchini Ufilipino, aliingizwa kazini katika Ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Lushoto na kisha yeye kumuingiza kazini Msaidizi wake, Mch. Michael Mlondakweli Kanju.

ILIVYOKUWA

Ibada ilianza kwa maandamano kutoka yalipo Makao Makuu ya Dayosisi hiyo, yaliyopo katikati ya Mji wa Lushoto na kuelekea Kanisa Kuu huku waki jipanga kwa kuongozwa na mbeba msalaba,

wabeba bendera ya Dayosisi na wapiga tarumbeta ambao walikuwa zaidi ya mia moja.Wapiga tarumbeta walikuwa kivutio kikubwa kwani walikuwa mahiri katika upigaji wao, pia walikuwa na sare ya pamoja ya mashati meupe na suruali nyeusi kwa wanaume na wanawake sketi nyeusi.

Hits: 15031

Read more ...

Taarifa ya mchango wa kukabiliana na deni la Dayosisi kwa mwezi April

  • Print
Details
Published: 01 May 2022

 

Uongozi wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kupitia kwa Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu umeanza utekelezaji wa ahadi waliyoitoa juu ya utaoji wa taarifa  ya  fedha zinazochangwa na Wanadayosisi zitakazo saidia kukabiliana na Deni la Dayosisi.

Ikumbukwe kua mnamo tarehe 24/03/2022 Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu aliwaandikia barua wana Dayosisi kuwaomba kuingia kazini ili kukabiliana na madeni makubwa yanayoikabili Dayosisi ambayo kwa ujumla wake ni hatarishi kwani yanaweza kusababisha mali za Dayosisi kupigwa mnada, kudumaza Dayosisi kwa muda mrefu, kutokuaminiwa na wadau wa maendeleo, kuathirika kwa Misioni pamoja na kufisha maono ya viongozi.

Hits: 14269

Read more ...

Uchimbaji wa madini waanza Vuga Kihitu

  • Print
Details
Published: 27 April 2022

 

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amezindua rasmi shughuli za uchimbaji wa madini Vuga Kihitu yaliyopo katika shule ya sekondari ya Bangala na kuwataka wachimbaji kufuata na kuheshimu sheria zilizowekwa ili kulinda na kudumisha amani.

Akimuwakilisha Askofu Dkt. Mbilu katika uzinduzi huo msaidizi wa Askofu Mch. Michael Kanju amesema kuwa uchimbaji huo unafanyika kwa mujibu wa sheria za Nchi hivyo kuwataka wachimbaji hao kutokuvunja sheria sambamba na kuwaasa kutambua eneo hilo ni sehemu ya kuwainua kiuchumi.

Hits: 14875

Read more ...

Ibada ya kuingizwa kazini kwa msaidizi wa Askofu KKKT-Dayosisi ya Mkoani Mara

  • Print
Details
Published: 24 April 2022

SEHEMU YA MATUKIO KATIKA PICHA, Ibada ya kuingizwa kazini kwa msaidizi wa Askofu KKKT-Dayosisi ya Mkoani Mara. Mch Eliya Kisarema Bwigeki iliyofanyika tarehe 24/04/2022, Msaidizi wa Askofu KKKT-DKMs, Mch Michael Mlondakweli Kanju alimuwakilisha Askofu wa KKKT-DKMs Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu katika Ibada hiyo.

Hits: 16736

Read more ...

  1. ASKOFU DKT. FREDRICK ONAEL SHOO KUFANYA ZIARA KKKT-DKMs
  2. Salamu za Pasaka za Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu
  3. Balozi Fanuel Kuzilwa azikwa nyumbani kwao Mlalo
  4. Ibada ya Mazishi ya Mzee Nicholas Mkala

Page 84 of 137

  • 79
  • ...
  • 81
  • 82
  • 83
  • 84
  • ...
  • 86
  • 87
  • 88

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese