ELCT North Eastern Diocese
Ibada ya Kipaimara KKKT-DKMs,Usharika wa Mshihwi
- Details

Msaidizi wa Askofu KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Michael Mlondakweli Kanju leo tarehe 21/05/2022 ameongoza Ibada iliyokuwa na tendo la kuwabariki vijana wa kipaimara katika Usharika wa Mshihwi Kanda ya Mto Umba Jimbo la Tambarare. Liturgia iliongozwa na Mkuu wa Jimbo hilo Mch. Frank Richard Mntangi.
- Hits: 15273
Askofu Dkt. Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Katibu wa maswala ya kimataifa wa Dayosisi ya Lund
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, akiwa katika mazungumzo na Katibu wa maswala ya kimataifa wa Dayosisi ya Lund- Sweden Bi. Marie Körner, mara baada ya kuwasili Makao Makuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Leo tarehe 14 Mei,2022.
- Hits: 14531
SIKU YA BWANA YA 4 BAADA YA PASAKA,"MWIMBIENI BWANA WIMBO MPYA" (KANTATE DOMINO)
- Details
SIKU YA BWANA YA 4 BAADA YA PASAKA
JUMAPILI YA TAR. 15 MEI, 2022
NENO KUU:
"MWIMBIENI BWANA WIMBO MPYA" (KANTATE DOMINO)
"Kila mwenye pumzi na Amsifu Bwana"
ZAB.147:7--11
7 Mwimbieni Bwana kwa kushukuru, Mwimbieni Mungu wetu kwa kinubi.8 Huzifunika mbingu kwa mawingu, Huitengenezea nchi mvua, Na kuyameesha majani milimani.9 Humpa mnyama chakula chake, Wana-kunguru waliao.10 Hapendezwi na nguvu za farasi, Wala hairidhii miguu ya mtu.11 Bwana huwaridhia wao wamchao, Na kuzitarajia fadhili zake.
SIKU YA BWANA YA NNE INAYOFUATA PASAKA
Mwimbieni Bwana wimbo mpya (Kantate Domino)
AYA YA SIKU
"Mwimbieni Bwana wimbo mpya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu" Zab.98:1
SALA
Mwenyezi Mungu, wewe peke yako waweza kuzitawala nia za waaminio kwa umoja; Uwajalie watu wako kupenda uliyoyaamuru na kutaka uliyoyaahidi, ili katika dunia hii isiyo na raha, mioyo yetu istarehe huko kwenye furaha ya kweli. Kwa Yesu Kristo, Mwana wako na Bwana wetu. Amen.
SOMO LA 1: 2 The. 2:13--17
13 Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu mliopendwa na Bwana, kwa kuwa Mungu amewachagua tangu mwanzo mpate wokovu, katika kutakaswa na Roho, na kuiamini kweli;14aliyowaitia ninyi kwa injili yetu, ili kuupata utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.15 Basi, ndugu, simameni imara, mkayashike mapokeo mliyofundishwa, ama kwa maneno, ama kwa waraka wetu.16 Na Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe, na Mungu Baba yetu, aliyetupenda akatupa faraja ya milele na tumaini jema, katika neema, 17awafariji mioyo yenu, na kuwafanya imara katika kila neno na tendo jema.
SOMO LA 2 MAHUBIRI:
Zab.104:33--35
33Nitamwimbia Bwana maadamu ninaishi; Nitamshangilia Mungu wangu nikiwa hai;34 Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake; Mimi nitamfurahia Bwana. 35 Wenye dhambi waangamizwe katika nchi, Watendao ubaya wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.
- Hits: 15432
Ziara ya kikazi Nchini Italy, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu
- Details

KATIKA PICHA Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, akiwa Nchini Italy na Torre Pellice ambapo viongozi mbalimbali wa dini wamekutana na kuhudhuria kozi ya uongozi iliyokuwa inahusu maswala ya Uhamiaji na tamaduni katika jamii (migration and multicultural society) iliyo ratibiwa na Kanisa la Waldensian (Waldensian Church) Kanisa mwanachana wa UEM Nchini ujerumani (partner church of the UEM in Germany).



- Hits: 13241
Page 83 of 137

