ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI YA KAZI Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya...
  • Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji  NSSF

    Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF

    Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifa...
  • TAARIFA

    TAARIFA

    Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, u...
  • ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Jos...
  • Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Dayosisi yetu imepata heshima kubwa ya kushiriki katika Mkutano wa Kanda ya Afrika ulioandaliwa na U...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

Askofu Dkt. Msafiri Mbilu aahidi kuboresha Maslahi kwa Wainjilisti

  • Print
Details
Published: 09 June 2022

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch. Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameahidi kusimamia Maslahi na kuboresha hali ya kiutumishi kwa kila Mwinjilisti aliyeajiriwa na Dayosisi ikiwemo kuwekewa michango katika mfuko wa hifadhi ya jamii na kwamba hakuna Mwinjilisti atakae staafu bila ofisi ya Askofu kujua.

Askofu Dkt. Mbilu ameeleza hayo leo tarehe 09/06/2022 wakati akifungua semina ya siku nne iliyoandaliwa kwa Wainjilisti  wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki yenye lengo la kuwajengea uwezo,inayofanyika   katika ukumbi wa mikutano wa  Benjamin Mkapa SEKOMU.

Hits: 16409

Read more ...

Mch. Geoffrey  Mwakihaba awekwa wakfu na kusimikwa kuwa Askofu wa awamu ya Tano KKKT-Dayosisi ya Konde

  • Print
Details
Published: 05 June 2022

 KATIKA PICHA: Ibada ya kuwekwa wakfu na kusimikwa kwa Askofu wa awamu ya Tano KKKT-Dayosisi ya Konde Mch. Geoffrey S. Mwakihaba, Ibada hiyo imefanyika leo tarehe 05/06/2022, katika Usharika wa Kanisa Kuu tukuyu-Mbeya

na kuongozwa na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kiluther Tanzania (KKKT) Askofu Dkt.Fredrick Shoo huku Liturgia ikiongozwa na Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch.Dkt. Msafiri Joseph Mbilu.

...............................

Hapo jana katika Ibada maalumu ya kuwekwa wakfu vifaa vya kiuaskofu iliyo ongozwa na Askofu Mstaafu wa Dayosisi hiyo  Askofu Dkt. Israel Peter Mwakyolile katika Usharika wa Kanisa Kuu tukuyu Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch.Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ndiye aliye hubiri katika Ibada hiyo.

Hits: 15243

Pumzika kwa amani Bibi,Hilgati A. Kika

  • Print
Details
Published: 30 May 2022

Ufunuo 14:13 “Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”.

 Leo tarehe 30/05/2022 imefanyika Ibada ya mazishi ya Marehemu  Bibi,Hilgati A. Kika katika Usharika wa Makorora Jimbo la Pwani. Marehemu Bibi,Hilgati  Kika katika uhai wake alikuwa muimbaji wa kwaya Kuu KKKT-DKMs Usharika wa Makorora.

 

Marehemu Bibi,Hilgati ambaye pia ni mama mdogo wa Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, mwili wake umepumzishwa katika makaburi ya Bombo area Jijini Tanga.

Marehemu Bibi Hilgati alizaliwa tarehe 01/07/1948 katika Kijiji cha Kwang’wenda Wilayani Lushoto aliitwa mbinguni alfajiri ya tarehe 28/05/2022 katika Hospitali ya Mkoa wa Tanga- Bombo.

Uongozi wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki unaendelea kutoa pole kwa,familia ya marehemu,Kwaya Kuu Makorora,   ndugu, jamaa na marafiki popote pale walipo. BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.

 

Hits: 13169

Askofu Dkt. Mbilu -Tuendelee kupunguza deni la Dayosisi

  • Print
Details
Published: 29 May 2022

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameendelea kuwa kumbusha Washarika wa Usharika wa Kange na Dayosisi kwa ujumla kuendela kuchangia Deni la Dayosisi na kusema kuwa taarifa ya michango hiyo itaendelea kutolewa kama ilivyo fanyika awali.

amewakumbusha Washarika hao leo tarehe 29/05/2022  ni siku ya Bwana kabla ya Pentekoste, SIKU YA CCT Neno Kuu (Sikia Kuomba kwetu) Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameongoza Ibada ya Jumapili katika Jimbo la Pwani Usharika wa Kange na kuwasihi Washarika na Wanadayosisi kuona umuhimu wa kutoa sadaka ya CCT.

Hits: 15249

Read more ...

  1. Ibada ya ndoa kati ya Mtheologia Jonathan Denisi Hiza
  2. Pumzika kwa amani Mzee Paul Kaijuka
  3. Mwaka mmoja wa Mch. Anderson Kipande
  4. Uzinduzi wa mwaka wa wanawake KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Jimbo la Pwani

Page 81 of 137

  • 76
  • 77
  • 78
  • 79
  • ...
  • 81
  • 82
  • 83
  • 84
  • ...

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese