ELCT North Eastern Diocese
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. TANGAZO LIMERUDIWA - RE- ADVERTISEMENT
- Details

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki imepata kibali cha ajira 6 za Watumishi wa Kada za afya kwa ajili ya Hospitali na vituo vya afya.
- Hits: 13297
Askofu Dkt. Mbilu ahesabiwa awasihi wana KKKT-DKMs kutoa taarifa sahihi
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu akizungumza na Karani wa Sensa ya Watu na Makazi wakati alipokuwa akihesabiwa na Karani wa Sensa ya Watu na Makazi ndugu Lazaro Henry Mnyawamikatika makazi yake Chatllon Lushoto Tanga leo Tarehe 23 Agosti, 2022 ambapo zoezi hilo lilimhusisha yeye mwenyewe, mke wake, vijana wake pamoja na watu wote waliolala kwenye makazi hayo.
- Hits: 12838
TANGAZO LA UDAHILI WA MUHULA MPYA WA MASOMO 2022/2023
- Details

Uongozi wa Chuo cha Kolowa Technical Training Institute (KOTETI) kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga, kinacho milikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki na chenye Usajili wa NACTE kwa No. KOTETI/HAS/249 unatangaza nafasi ya masomo kwa muhula mpya wa SEPTEMBER-2022/2023 kwa kozi ya PHARMACY.
- Hits: 14057
ASKOFU DKT. MSAFIRI MBILU: Msiyumbishwe na mafundisho potofu ya neno la Mungu.
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewataka Washarika wa Usharika wa Mikanjuni na Wakristo kwa ujumla kuepukana na mafundisho potofu ya neno la Mungu na badala yake kuendelea kumtegemea Mungu katika Maisha yao.

Askofu Dkt. Mbilu ametoa wito huo leo tarehe 21/08/2022 katika Ibada ya Jumapili iliyokuwa na tendo la kuwabariki vijana wa kipaimara wapatao 27 iliyofanyika katika Usharika wa Mikanjuni Jimbo la Pwani ambapo amesema kwa siku za hivi karibuni Wakristo wamekuwa wakiyumbishwa na kuvutwa na mafundisho ya uongo hivyo kuzitaka Sharika kuandaa Semina za ujasiriamali ili washarika wapate fulsa ya kujifunza namna bora ya kujikwamua kiuchumi.

Kwa upande wake Msaidizi wa Askofu KKKT-DKMs Mch. Michael Kanju ambaye ndiye aliye hubiri katika Ibada hiyo amewakumbusha washarika na wakristo kwa ujumla kutumia vyema nafasi zao kwa kutenda haki kwa kila mtu na kuishi maisha ya kumtegemea Mungu zaidi.

Hata hivyo Askofu Dkt. Mbilu ameendelea kuwakumbusha Washarika na watu wote kwa ujumla kujiandaa na zoezi la Sensa ya watu na makazi itakayo fanyika tarehe 23/08/2022 . Umuhimu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 ni pamoja na Kuisaidia Serikali kupata taarifa za msingi zitakazosaidia mchakato wa utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025.

mageuzi ya masuala ya afya na jamii, pamoja na ufuatiliaji wa ajenda za maendeleo za kimataifa; Taarifa za idadi ya watu husaidia katika mamlaka za Wilaya katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ambayo huakisi matakwa ya watu katika ngazi husika na kusaidia kwenye uwiano wa mgawanyo wa rasilimali.

- Hits: 14353
Page 74 of 137

