ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI YA KAZI Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya...
  • Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji  NSSF

    Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF

    Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifa...
  • TAARIFA

    TAARIFA

    Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, u...
  • ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Jos...
  • Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Dayosisi yetu imepata heshima kubwa ya kushiriki katika Mkutano wa Kanda ya Afrika ulioandaliwa na U...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

IBADA YA KIPAIMARA KKKT-DKMs, Jimbo la Kaskazini,Usharika wa Mlalo.

  • Print
Details
Published: 17 July 2022

Leo tarehe 17/07/2022 imekuwa siku ya baraka tele kwa washarika wa Jimbo la Kaskazini ,Usharika wa Mlalo kwani vijana wapatao 116 walipata kipaimara na wanne  4 kati yao walibatizwa.

Katika Ibada hiyo Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ndiye aliye ongoza Ibada hiyo, huku Liturgia ikiongozwa na Msaidizi wa Askofu KKKT-DKMs Mch. Michael Mlondakweli Kanju. 

 Katika Risala ya vijana hao waliobarikiwa iliyosomwa mbele ya Baba Askofu Dkt. Msafiri Mbilu vijana hao wametambua jitihada za Baba Askofu pamoja na wasaidizi wake katika kusimamia mambo ya Elimu na Afya.  Hata katika kipindi hiki ambacho Dayosisi inakabiliana na  deni  bado wameona na kushuhudia kazi za maendeleo zikiendelea kufanyika.

Wameeleza kujisikia fahari kuona shule za Dayosisi (Lwandai na Bangala) zikiboreshwa na kuvutia wanafunzi wengi zaidi. Huku wakitambua jitihada za kukifufua kilichokuwa Chuo cha SEKOMU,kwa hatua za awali za kuanzishwa kwa Chuo cha Kati cha Kolowa Technical Training Institute (KOTETI) kitakachotoa kozi ya famasia.

Hits: 13134

Katika picha Ibada ya Jumapili Usharika wa Ngwelo “B” Bumbuli,

  • Print
Details
Published: 10 July 2022

KATIKA PICHA: Ibada ya Jumapili kutoka Jimbo la Kusini Usharika wa Ngwelo “B” Bumbuli, ambapo Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ndiye aliyeongoza Ibada hiyo leo tarehe 10/07/2022.

Msaidizi wa Askofu Mch. Michael Mlondakweli Kanju

Mkuu wa Jimbo la Kusini Mch. Issai Mweta

 

Hits: 12673

Happy Saba Saba Day!

  • Print
Details
Published: 07 July 2022

Happy Saba Saba Day! Tanzania census August 2022 prepare to be counted

Hits: 14521

Askofu Mbilu awashukuru wana KKKT-DKMs

  • Print
Details
Published: 03 July 2022

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs), Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewashukuru wanadayosisi na wote walioshiriki katika maombi ya kumuombea mwenzi wake Mwl. Mary Mbilu katika kipindi chote cha kuugua kwake.

Ametoa shukrani hizo katika Ibada maalumu ya kumshukuru Mungu kwa kumponya na kumvusha katika kipindi kigumu cha kuugua kwa mwenzi wake na kusema kuwa maombi na sala za wanadayosisi ndugu jamaa na marafiki yamekuwa faraja kwao na kuwaomba kuendelea kuikumbuka familia hiyo katika maombi.
Katika hatua nyingine Askofu Dkt. Mbilu amewahimiza waumini na wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi katika zoezi la sensa ya watu na makazi ambayo inatarajiwa kufanyia mwezi Agosti,2022 kwa lengo la kupata takwimu sahihi kwa maendeleo ya Taifa kwa ujumla huku ikiongozwa na kauli mbiu isemayo: SENSA KWA MAENDELEO, JIANDAE KUHESABIWA

 


Aidha kwa upande wake Mwl. Christopher Mwakasege ambaye ndiye aliyehubiri neno la Mungu katika Ibada hiyo maalumu ya Shukrani iliyofanyika Kanisa Kuu Lushoto, amewataka waumini kujijengea tabia ya kumshukuru Mungu kwa matendo makuu anayowatendea kwani kwakufanya hivyo wanampa nafasi Mungu kuzidi kutenda miujiza juu yao.


Ibada hiyo ya Shukrani pia imehudhuriwa na Askofu Mstaafu wa KKKT-DKMs Mzee Joseph Jali,viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Mhe. Kalisti Lazaro,Diwani wa Lushoto Mjini,Mkurugenizi wa Halmalmashauri ya Lushoto pamoja na ndugu jamaa na marafiki kutoka ndani na nje ya Dayosisi.

Hits: 12873
  1. Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,afanya mazungumzo na Dkt. Charles Mhina
  2. Tangazo la nafasi za kazi
  3. JOB VACANCY ANNOUNCEMENT- GENERAL SECRETARY OF ELCT-NORTH EASTERN DIOCESE
  4. Askofu Dkt. Msafiri Mbilu akutana na kufanya mazunguzo na mtaalamu wa maswala ya utawala katika biashara na viwanda

Page 78 of 137

  • 73
  • 74
  • ...
  • 76
  • 77
  • 78
  • 79
  • ...
  • 81
  • 82

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese