ELCT North Eastern Diocese
ASKOFU DKT. MBILU: Tujifunze kuomba kwa usahihi.
- Details

Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amewakumbusha Washarika wa Usharika wa Kana na Wakristo kwa ujumla, kuendelea kuomba neema ya Mungu iwaongoze katika kuomba kwa usahihi kama Kristo Yesu alivyo wafundisha wanafunzi wake katika Sala ya Bwana.
Askofu Dkt. Mbilu ametoa wito huo leo tarehe 14/05/2023 wakati akihubiri katika Ibada ya Jumapili ya tano baada ya Pasaka (Rogate) iliyofanyika katika Jimbo la Pwani Usharika wa Kana, ambapo amesema kwa sasa kumekuwa na uwepo wa walimu wanaofundisha mafundisho potofu yanayo wafanya Wakristo kushindwa kuomba kwa usahihi.
- Hits: 13174
Mkutano wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani,kanda ya Afrika
- Details

KATIKA PICHA ni Ujumbe kutoka Tanzania uliohudhuria Mkutano wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani. Katikati ni Mkuu wa KKKT Askofu Dkt. Fredrick Shoo, kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa LWF Mch. Dkt.. Anne Burghadt akifuatiwa na Rais wa LWF Archibishop Musa Panti Filibus.
- Hits: 11623
Miaka miwili ya Uongozi wa Askofu Dkt. Mbilu awashukuru wana KKKT-DKMS
- Details

Mei 9 mwaka 2021 ilikuwa ni siku iliyotawaliwa na nderemo, vifijo na shamrashamra katika viunga vya Lushoto, siri nyuma ya furaha hii si nyingine bali ni historia mpya kuandikwa, wakristo wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki walipata Askofu mpya, kiongozi ambae atayabeba maono na dira ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki huyu sio mwingine bali ni Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu.Mhadhiri huyo mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Silliman cha nchini Ufilipino, aliingizwa kazini katika Ibada iliyofanyika Kanisa Kuu Lushoto tarehe 09/05/2021 na kisha yeye kumuingiza kazini msaidizi wake, Mch. Michael Mlondakweli Kanju.
- Hits: 10382
Kauli ya Mkuu wa KKKT juu ya Ubadhirifu Serikalini
- Details

MKUU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dkt. Fredrick Shoo, ameishauri serikali kushughulikia kwa ukali tuhuma za ubadhirifu zinazosikika kuiandama miradi mikubwa yenye manufaa kwa taifa. Askofu Dkt. Shoo pia amesema Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania haliungi mkono vitendo vya ushoga na ndoa za jinsia moja na halitoacha kutumia rangi za upinde wa mvua kwenye nembo yake kwa kuwa "ni agano la Mungu".
- Hits: 10310
Page 54 of 137

