ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • TAARIFA

    TAARIFA

    Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, u...
  • ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Jos...
  • Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Dayosisi yetu imepata heshima kubwa ya kushiriki katika Mkutano wa Kanda ya Afrika ulioandaliwa na U...
  • Contact Us

    Contact Us

    SOUTHERN SUPERINTENDENT BARUA PEPE JIMBO LA KUSINI southern.superintendent@elctned.org cathedral@elc...
  • Askofu Dkt. Mbilu afungua Kikao Kazi cha Tathmini ya Mwaka 2025

    Askofu Dkt. Mbilu afungua Kikao Kazi cha Tathmini ya Mwaka 2025

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Jos...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

Pumzika kwa Amani Bibi. Elise David Ngome

  • Print
Details
Published: 28 January 2025
Ufunuo 14:13“Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao”.
 
KATIKA PICHA:Ibada ya mazishi ya Bibi. Elise David Ngome, iliyofanyika leo tarehe 28/01/2025 katika Jimbo la Kusini Usharika wa Mgwashi na kuongozwa na msaidizi wa Askofu KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch. Michael Mlondakweli Kanju akishirikiana na Mkuu wa Jimbo la Kusini Mch. Issai Mweta.
Hits: 7124

Read more ...

Matokeo kidato cha nne Shule ya Lwandai na Bangala zafanya vizuri Askofu Dkt. Mbilu asema zimewapa raha wana KKKT-DKMS

  • Print
Details
Published: 23 January 2025

Shule za Sekondari za Lwandai na Bangala Junior Seminary, zinazomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs), zimeendelea kufanya vizuri katika matokeo  ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika November, 2024

 Katika matokeo hayo, shule ya Lwandai imevutia zaidi baada ya kutoa mwanafunzi aliyepata alama za juu akiwa na daraja la kwanza lenye pointi saba (One ya 7), kitu kinachoashiria uwekezaji mkubwa katika elimu bora na juhudi za walimu pamoja na wanafunzi.

  Kufuatia matokeo hayo Askofu wa KKKT-DKMs, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ,ametoa pongezi kwa walimu na wafanyakazi wa Shule hizo kwa kazi nzuri walioifanya huku akiahidi kuendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia ili kuweka msingi imara wa mafanikio zaidi ya siku zijazo.

 Kakita hatua nyingine Askofu Dkt. Mbilu, ametoa shukrani zake za dhati kwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Dayosisi kwa kukubali ombi la kila Usharika wa KKKT-DKMS kusomesha mwanafunzi mmoja katika Shule hizi.

 “ninapoyatazama matokeo haya ya kishindo ya Shule zetu Lwandai na Bangala ninajikuta mdomo wazi nikimshangaa Mungu kwa jambo hili kubwa alilotutendea. Ninawapongeza ninyi wote kwa maamuzi yale magumu tuliyofanya kwenye kikao chetu cha kwanza cha tarehe 17.12.2020 kuwa kila Usharika usomeshe mwanafunzi mmoja kuanzia Januari 2021 ili kuondoa aibu ya Shule hizi kuwa na wanafunzi wachache wa kidato cha kwanza Lwandai 8 na Bangala 3. Hili limezaa matunda haya na kwa hakika Shule zetu zimefufuka. Hongereni sana.

 Siku chache kabla ya Mtihani wa kidato cha Nne nilitembelea Shule zetu hizi kufanya maombi na watoto wetu na kuwapa kila mmoja kalamu ya kufanyia Mtihani kwa niaba yenu. Hakika Mungu amesikia maombi yetu na ametenda na ameamua KUTUPA RAHA. Nawapongeza ninyi Wajumbe wa Halmashauri Kuu, Wana KKKT-DKMS na wadau wote wa maendeleo  kwa Ufadhili wao.

Nawapongeza Wazazi wa watoto hawa, Nawapongeza Wakuu wa Shule zetu, Walimu wote na watenda kazi wote kwa ufaulu huu wa hali ya juu sana. Tunazo hadi Divisheni One ya point 7. Nawapongeza watoto wetu kwa kufanya vizuri kwenye Mtihani Huu”Amesema Askofu Dkt. Mbilu.

 Pamoja na hayo Askofu Dkt. Mbilu, amempogeza kipekee mwanafunzi Helena Frank Kaduma wa shule ya sekondari Lwandai kwa kupata ufaulu wa Division One ya point 7 ambapo mwanafunzi huyo amesomeshwa na Usharika wa Hale pamoja na mwanafunzi kutoka shule ya seminari ndogo ya Kilutheri Bangala,Dickson David Kika ambaye amepata ufaulu wa Division one ya 9 ambaye amesomeshwa na usharika wa Soni.

Matokeo haya mazuri yanaendeleza sifa nzuri ya shule hizi kama vituo vya elimu vinavyozalisha viongozi wa kesho walio na maarifa na maadili mema, na ujuzi unaohitajika kwa maendeleo ya Taifa. Sharika za KKKT-DKMS zitaendelea kuwasomesha vijana hawa kidato cha Tano na cha Sita. Mungu aendelee kutubariki tunapoyafanya makubwa haya. "BWANA AKASEMA, USO WANGU UTAKWENDA PAMOJA NAWE, NAMI NITAKUPA RAHA"(Kutoka 33:14).

Hits: 7657

Uanzishwaji wa kozi ya muziki KOTETI maandalizi yanaendelea vizuri

  • Print
Details
Published: 22 January 2025

HABARI KWA UFUPI: Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,amesema kuwa mipango ya uanzishwaji wa kozi ya muziki katika Taasisi ya Elimu ya Kolowa Technical Training Institute (KOTETI) inaendelea vizuri ikiwa ni pamoja na vifaa vitakavyo tumika katika kufundishia kuanza kupatikana.

Askofu Dkt. Mbilu ameyasema hayo leo tarehe 22/01/2025 akiwa katika Ofisi za Makao Makuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki yaliyopo Wilayani Lushoto Mkoa wa Tanga, mara baada ya kupokea ugeni wa marafiki kutoka Bethel Ujerumani.

Ugeni huu unaongozwa na Bw.Werner Jakob Blauth, ambaye alishaawahi kufanya kazi katika kituo cha Lutindi Mental Hospital kinachomilikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.

Aidha Askofu Dkt. Mbilu, ameongeza kuwa ugeni huo umetembelea KKKT-Dayosisi Kaskazini Mashariki kwa lengo la kuona baadhi ya vituo vya Diakonia vya Dayosisi ikiwemo kituo cha Irente children's Home, Irente Rainbow School, Irente School for the Blind pamoja na Hospital ya wagonjwa wa akili (Lutindi Mental Hospital) ili kujionea shughuli mbalimbali zinazofanyika katika vituo hivyo.

Vifaa vilivyo pokelewa leo ni pamoja na Tarumbeta filimbi vikiwa ni alama tu ya vifaa vingine vingi vya muziki ambavyo vipo nchini Ujerumani vikiwa katika hatua za mwisho kusafirishwa kuja katika Dayosisi yetu.

Hata hivyo Askofu Dkt. Msafiri Mbilu, amewashukuru wageni hao kwa mchango wao mkubwa wa kutoa vifaa hivyo vya muziki ikiwa ni ishara ya kuendelea kuonyesha ushirikiano mzuri uliopo kati ya Dayosisi na marafiki hao kutoka Ujerumani.

Hits: 6707

Kuelekea Ibada ya kuwekwa wakfu Askofu wa KKKT-Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria (Mwanza)

  • Print
Details
Published: 18 January 2025
KATIKA PICHA: Ibada illiyokuwa na tendo la kuweka wakfu vifaa vya kiaskofu iliyofanyika KKKT-Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria (Mwanza) Usharika wa Imani Kanisa Kuu. Ibada hii iliongozwa na Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu.
Hits: 7853

Read more ...

  1. Picha ya pamoja mara baada ya Mkutano wa Halmashauri ya Utumishi ya KKKT
  2. Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi aitembelea KKKT-DKMs
  3. HERI YA MWAKA MPYA 2024
  4. Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Kuu ya KKKT-DKMs watembelea kituo cha Irente Children's Home pamoja na Irente School for the Blind

Page 13 of 136

  • 8
  • 9
  • ...
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • ...
  • 16
  • 17

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese