ELCT North Eastern Diocese
MWANGAZA Educational Center program Coordinators watembelea Ofisi za KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.
- Details
Mwangaza program coorinators leo tarehe 10/03/2021 wamepata nafasi ya kutembelea Makao Makuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki lengo likiwa ni kutembelea shule za sekondari za Dayosisi.

Katika picha ni ,Mwl.John Kavishe wa kwanza kutoka kushoto,Mr.Richard Mbwambo wa pili kutoka Kushoto,Mch.Joyce Kibanga Mkurugenzi wa huduma za jamii wa tatu kutoka kushoto na Bi.Salome Lally wa nne kutoka kushoto. Kutoka kulia ni Bw. David Chanyeghea Kaimu Mkurugenzi Uchumi,Mipango na Maendeleo, Kaimu Katibu Mkuu Mch.Godfrey Walalaze wa pili kutoka kulia, Dean Mteule Mch. Michael Kanju wa tatu kutoka kulia na Askofu. mteule Mch.Dkt.Msafiri Joseph Mbilu wa tano kutoka kulia.
- Hits: 16087
KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki yafanya Uzinduzi wa Harambee kubwa yenye lengo la kuimarisha Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa SEKOMU.
- Details

Askofu Mteule wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch.Dkt.Msafiri Joseph Mbilu amejumuika na Washarika wa Usharika wa Kana katika Ibada ya Jumapili ambapo Ibada hiyo pamoja na kuwa na matukio mbalimbali kumekuwa na Uzinduzi wa Harambee yenye lengo la kuchangisha jumla ya Sh 2,000,000,000 (Bilioni Mbili) ili kuimarisha Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa SEKOMU.

Katika Hotuba yake aliyoitoa kwa mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe Martin Shigela, Askofu Mteule Mch.Dkt. Mbilu alisema imekuwa siku ya furaha kubwa kutembelewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga ambapo alimkaribisha Mkuu huyo wa Mkoa katika Usharika wa Kana na Dayosisi kwa ujumla.
Askofu Mteule Mch.Dkt. Mbilu amesema kuwa katika kipindi cha takribani miaka 3 kumekuwa na changamoto kubwa ya Chuo kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa SEKOMU, kufungiwa udahili kutoka na matatizo mbalimbali ya kimfumo na yaki utendaji.Hata hivyo baada ya Uongozi mpya wa Dayosisi kuingia madarakani mwezi Novemba 2020 uongozi umejikita sana katika kuhakikisha Chuo Kikuu cha SEKOMU kinasimama tena.

- Hits: 18546
Ziari ya Askofu Mteule Mch.Dkt.Msafiri Joseph Mbilu na Kaimu Katibu Mkuu Mission ya Kigoma
- Details

Askofu Mteule Mch. Dkt. Msafiri J. Mbilu yupo ziarani katika Mission ya Kigoma ambapo ameshiriki katika kikao cha maandalizi ya Mission hiyo inayoandaliwa kuwa Dayosisi.

Askofu Andrew Petrol Gulle na Katibu Mkuu Bw. Rigath Mille wa KKKT- Dayosisi Mashariki ya Ziwa Victoria na Askofu Dkt.Abednego N. Keshomshahara na Katibu Mkuu Mch. Elimerek Kigembe wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Magharibi pia wameshiriki katika kikao hicho.
- Hits: 18160
Wahitimu wa mafunzo ya Muziki Kanisa Kuu Lushoto
- Details

Wahitimu wa Muziki (Tarumbeta) wakiwa katika picha ya pamoja na mwalimu wao ndugu Michael Kivulenge wa kwanza kutoka kulia mara baada ya Ibada Kanisa Kuu Lushoto. Leo tarehe 21/02/2021
- Hits: 16719
Page 119 of 137

