ELCT North Eastern Diocese
Salamu za Pasaka,Askofu Mteule Mch.Dkt.Msafiri Joseph Mbilu KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki,
- Details

Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa. Hayupo hapa; kwani amefufuka kama alivyosema (Mt. 28:5-6).
Wapendwa katika Bwana, kufufuka kwa Yesu ni tukio la imani kubwa kwetu sote tunaoamini juu ya nguvu ya ufufuo. Tukio hili linaondoa hofu inayotanda mioyoni mwa wengi juu ya kifo na nguvu ya mauti.
Tunasherehekea Pasaka wakati ambapo mioyo ya wengi imejawa na hofu kubwa ya magonjwa ya kutisha yanayosikika mahali pote duniani, misiba ya kutisha ya kuondokewa na wapendwa wetu. Haya yote yanatuletea mahangaiko na majonzi.
Katikati ya haya yote tunapokea ujumbe mkubwa wa matumaini Malaika anaposema “msiogope”.Tangazo hili la Malaika la kutuondolea hofu linaleta tumaini kubwa kwamba yupo mtangulizi ambaye ameshinda kifo na nguvu ya mauti. Yesu mfufuka analeta tumaini la kutokuogopa kifo na nguvu ya mauti kwetu tunaoamini. Kufufuka kwake hakujatokea kwa bahati mbaya bali ni mpango kamili wa Mungu katika historia ya ukombozi wetu sisi wanadamu. Hii ndiyo maana malaika anakiri akisema “amefufuka kama alivyosema”.
Tuitegemee nguvu ya Mungu iliyomfufua Yesu kuwa sasa tunaye mshindi aliyetutangulia na kwamba sisi sote tunaomwamini hatuna sababu ya hofu ya mauti kwani Bwana amefufuka kutoka kwa wafu.
Huyu Yesu aliyefufuka akaendelee kutujaza matumaini mapya, kwetu mmoja mmoja, matumaini katika familia zetu na jamii kwa ujumla.

....................................................................................

- Hits: 16661
Msaidizi wa Askofu KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch.Michael Mlondakweli Kanju afungua mkutano Mkuu wa umoja wa Wanawake wachungaji.
- Details

Msaidizi wa Askofu Mteule wa KKKT- Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch.Michael Mlondakweli Kanju amewapongeza Wachungaji wanawake wa Dayosisi ya Kaskazini Mashariki kwa umoja wao katika kusaidiana,Kuhamasishana, kutembeleana katika maeneo yao ya kazi pamoja na kuombeana, kwa kuwa ni wito walioitiwa.
- Hits: 2126
Askofu Mteule wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (DKMs), kutembelea Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP) tarehe 28/03/2021
- Details

Askofu Mteule wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch. Dkt. Msafiri Joseph Mbilu pamoja na viongozi wengine wa Dayosisi watatembelea Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP) tarehe 28/03/2021 ambapo watashiriki na kuongoza Ibada katika baadhi ya sharika za DMP.
- Hits: 17143
Page 117 of 137


