ELCT North Eastern Diocese
Toggle Navigation
  • Home
  • Our Diocese
  • Wopa
  • Gallery
  • Institutions
    • Irente Children's Home
    • Irente School for the Blind
    • Rainbow School
    • Lwandai Secondary School
    • Lutindi Mental Hospital
    • Bangala Lutheran Junior Seminary
    • Bumbuli Hospital
    • SEKOMU university
    • Namna ya kuchangia kazi za maendeleo na Vituo vya kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu (KKKT-DKMs)
  • Calendar
  • Projects
    • Irente Biodiversity Reserve
    • UTC - Usambara Technological Center
    • Restaurants and Hostels
      • Tumaini Mbuyukenda Hostel and Restaurant
      • Martin Luther Garden and Restaurant
      • Tumaini Songe Restaurant and Hostel
      • Hohen Restaurant and Hostel
      • Tumaini Lushoto Restaurant and Hostel
  • Superintendent
    • Coast Superintendent
    • Northern Superintendent
    • Southern Superintendent
    • Plains Superintendent
  • New-clips
  • Contact us
  • You are here:  
  • Home

Bishop Rev.Dr. Msafiri J. Mbilu

Change Language

English German Spanish Swahili Swedish

News & Updates

  • TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI MOJA YA KAZI MENEJA WA SHAMBA (FARM MANAGER) KITUO CHA IRENTE FARM

    TANGAZO LA NAFASI YA KAZI Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya...
  • Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji  NSSF

    Askofu Dkt.Mbilu akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Uendeshaji NSSF

    Leo tarehe 01/04/2026, Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amepokea ugeni kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifa...
  • TAARIFA

    TAARIFA

    Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, u...
  • ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Jos...
  • Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika

    Dayosisi yetu imepata heshima kubwa ya kushiriki katika Mkutano wa Kanda ya Afrika ulioandaliwa na U...

.



 

 

Staff Email

ELCT North Eastern Diocese

TANGAZO LA KAZI MTEKNOLOJIA DARAJA II-DAWA

  • Print
Details
Published: 17 November 2023

KANISA LA KINJIILI LA KILUTHER TANZANIA

DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI

S.L.P 10,

LUSHOTO.

 

 NAFASI YA KAZI

Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) ni miongoni mwa Dayosisi 27 ndani ya KKKT. Dayosisi inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-DKMs ni taasisi ya kidini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu. Taasisi hii inatoa tangazo la kazi kwa nafasi ifuatayo:

 

MTEKNOLOJIA DARAJA LA II-DAWA (NAFASI 1)

MAJUKUMU YA MUOMBAJI

  1. Kuanisha, kuandaa na kuagiza mahitaji ya dawa na vifaa tiba katika eneo la kazi.
  2. Kugawa dawa na vifaa tiba kwa wagonjwa na watumishi.
  3. Kuchanganya dawa.
  4. Kuhifadhi dawa na vifaa tiba.
  5. Kuelimisha jamii juu ya matumizi sahihi ya dawa.
  6. Kukagua dawa, vifaa tiba kemikali, vitendanishi na vipodozi katika eneo lake la kazi.
  7. Kutoa taarifa juu ya madhara yatokanayo na matumizi ya dawa.
  8. Kuratibu kazi za kamati ya dawa na vifaa tiba.
  9. Kuandaa taarifa ya matumizi ya dawa na vifaa tiba.
  10. Kufanya uchunguzi wa ubora wa dawa, vifaa tiba kemikali, vitendanishi na vipodozi.
  11. Kufanya kaguzi mbalimbali katika sehemu zinazohifadhi dawa.
  12. Kusimamia utendaji kazi watumishi walio chini yake.
  13. Kutunza kumbukumbu za dawa na vifaa tiba.

 SIFA ZA MWOMBAJI

  • Elimu ya kuanzia Diploma ya ufamasia kutoka chuo kinachotambuliwa na serikali.
  • Lazima
  • Ajue kutumia software za computer Zaidi kipengele cha Microsoft office.
  • Ajue kutumia software zinatumika katika usimamiaji wa dawa.
  • Mwenye moyo wa kufanya kazi kwenye mazingira yoyote.
  • Umri kuanzia miaka 25 na isiyozidi 40

 NAMNA YA KUTUMA MAOMBI.

  1. Barua ya maombi iambatanishwe na nakala za vyeti vya Elimu, wasifu wa mwombaji (Cv), cheti cha kuzaliwa, na nakala za vyeti vyote vya ujuzi mbalimbali (kama unavyo).
  2. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 24/11/2023
  3. Waombaji watakaokidhi vigezo ndio watakaoitwa kwenye usaili (Interview)

Tarehe ya usaili watajulishwa kwa njia ya simu.

 Maombi yote yatumwe kwa  Katibu Mkuu-KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki S.L.P 10 LUSHOTO Au: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

 

 

 

 

 

Hits: 10217

Ibada ya Kipaimara Usharika wa Ubiri , Youths Confirmation at Ubiri Lutheran Parish

  • Print
Details
Published: 12 November 2023
Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,Tarehe: 12/11/2023, akiwa katika Jimbo la Kusini, Usharika wa Ubiri, ameongoza Ibada iliyokuwa na tendo la kuwabariki Vijana wa Kipaimara.
Ambapo jumla ya Vijana wapatao 29 wamebarikiwa na 3 kati yao wamebatizwa, wakisoma Risala yao mbele ya Baba Askofu Dkt. Msafiri Mbilu vijana hao wamemshukuru Baba Askofu Dkt Msafiri Mbilu kwa kufika na kuungana nao katika siku ya kubarikiwa kwao na wamempongeza Baba Askofu kwa jitihada zake katika kuiongoza na kuiletea maendeleo Dayosisi.
Wameongeza kuwa wana tambua kazi kubwa inayofanywa na KKKT-DKMs katika kumhudumia mwanadamu kiroho, kimwili na kiakili hasa kazi kubwa inayofanyika katika kufufua na kuimarisha vituo vinavyotoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu
.
Katika Ibada hiyo Vijana hao walitoa kiasi cha Tsh 90,000 kwaajili ya kuchangia ulipaji wa deni la Dayosisi, ambapo pia waliomba kuungwa mkono na wazazi,walezi pamoja na washarika walioshiriki katika Ibada hiyo na kufanikiwa kukusanya jumla ya Ths. 1,312,700/= ambapo fedha hizo zimeelekezwa katika kulipa deni la Dayosisi.
Hits: 9273

Ibada ya Kipaimara Usharika wa Ambangulu , Youths Confirmation at Ambangulu Lutheran Parish

  • Print
Details
Published: 11 November 2023
Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu,Tarehe: 11/11/2023, akiwa katika Jimbo la Kusini, Usharika wa Ambangulu, ameongoza Ibada iliyokuwa na tendo la kuwabariki Vijana wa Kipaimara.
Ambapo jumla ya Vijana wapatao 62 wamebarikiwa na wawili kati yao walibatizwa, wakisoma Risala yao kwa Baba Askofu Dkt Msafiri Mbilu, wameeleza kuwa moja ya mafanikio waliyoyapata katika kipindi cha miaka 2 katika darasa lao la Kipaimara ni pamoja na kuandaliwa vema kiimani.
Wameongeza kuwa ili kumshinda mwovu shetani na hila zake wataendelea kusimama katika Imani, kujifunza neno la Mungu kwa kulisoma na kutembea nalo katika maisha yao huku wakiitegemea neema ya Mungu katika kuyatenda mapenzi yake.
 
Katika Ibada hiyo Vijana hao walitoa kiasi cha Tsh 200,000 kwaajili ya kuchangia ulipaji wa deni la Dayosisi, ambapo pia waliomba kuungwa mkono na wazazi,walezi pamoja na washarika walioshiriki katika Ibada hiyo na kufanikiwa kukusanya jumla ya Ths. 1,198,000/= ambapo fedha hizo zimeelekezwa katika kulipa deni la Dayosisi.
Hits: 8922

Kuelekea kilele cha kuchangia Deni la Dayosisi kwa awamu ya Tsh. 30,000 kwa kila Msharika wa KKKT-DKMs

  • Print
Details
Published: 05 November 2023

Kuelekea kilele cha uchangiaji wa Tsh 30,000 kwa kila msharika wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki-(KKKT-DKMs) kwa ajili ya kupunguza deni linaloikabili Dayosisi kitakacho fanyika katika Jimbo la Tambarare Usharika wa Korogwe tarehe 17/12/2023. Askofu Dkt Msafiri Mbilu amewashukuru wale wote ambao wameingia kazini kuchangia deni hilo.

Askofu Dkt. Mbilu ameongeza kuwa siku hiyo itakuwa ni kilele cha kukusanya kiasi hicho na kupata taarifa za uchangiaji kwa kila Usharika “Awali ya yote napenda kuwashukuru ninyi wote kwa jinsi mlivyopokea wito huu wa kila mmoja kuchangia Tsh. 30,000/=. Fedha hizi zimesaidia sana kupunguza deni la Dayosisi. Ninapenda kuwajulisha kuwa tutakuwa na siku rasmi ya kilele cha mchango huu wa Tsh. 30,000 tarehe 17/12/2023 kwenye Jimbo la Tambarare Usharika wa Korogwe, wapo watu wengi waliomaliza na kuendelea kuongeza zaidi na zaidi patano la kuchangia kiasi cha Tsh.30,000, lakini pia wapo ambao wameanza lakini hawajakamilisha nawasihi kukamilisha patano letu".Alisema  Askofu Dkt. Mbilu.

Baba Askofu amesisitiza kwa wale wote ambao bado hawajakamilisha mchango wa Tsh. 30,000/= wanaombwa kukamilisha mchango wao kupitia Sharika zao ili siku ya kilele taarifa ya kila Usharika iwasilishwe bila deni, ili kutoa mwanga wa jinsi ya kujipanga na awamu nyingine za uchangiaji.

Kutokana na ukubwa wa deni la Dayosisi harambee hizi zitakuwa endelevu,Baba Askofu anazidi kuwatakia baraka za Mungu ninyi nyote kwa kujitoa kwenu ili kazi ya Mungu iendelee kusonga mbele kwani kwa mshikamano uliopo ipo siku deni hili litakwisha na kurudisha heshima ya Dayosisi yetu.

Hits: 10160
  1. Askofu wa KKKT-DKMs Dkt. Msafiri Mbilu apokea wadiakonia 30 kutoka Ujerumani
  2. Pumzika kwa amani Mchungaji Mpewa Lazaro Ruwa
  3. Ziara ya Rais wa Ujerumani, Frank-Walter Steinmeier, nchini Tanzania.
  4. Ibada ya Kipaimara Usharika wa Tamota, Youths Confirmation at Tamota Lutheran Parish

Page 42 of 137

  • 37
  • 38
  • 39
  • ...
  • 41
  • 42
  • 43
  • 44
  • ...
  • 46

Back to Top

© 2026 ELCT North Eastern Diocese