ELCT North Eastern Diocese
TAARIFA
- Details

Uongozi wa KKKT – Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ukiwakilishwa na Katibu Mkuu Mwl. Julius Madiga, umefanya hafla ndogo ya makabidhiano ya mradi wa maji (Mazi kwa Woshe) tarehe 10/03/2026 katika ofisi ya Afisa Tarafa-Mnazi.
Lengo kuu la hafla hiyo lilikuwa ni mkandarasi mjezi wa kampuni ya Ntama and faith company lmtd, kukabidhi rasmi mradi huo kwa Dayosisi, na baadaye Dayosisi kupitia Katibu Mkuu kukabidhi mradi kwa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) pamoja na Kamati ya Maji ya UMBAWASO kwa ajili ya uendeshaji na usimamizi wake.
- Hits: 2543
ASKOFU KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI MASHARIKI AZINDUA BODI YA MFUKO WA PENSION
- Details

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki. Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, leo tarehe 04 Machi 2026, amezindua rasmi Bodi ya Mfuko wa Pension iliyochaguliwa na Halmashauri Kuu ya Dayosisi.
- Hits: 2527
Taarifa Ziara ya Botswana kwenye Mkutano wa UEM Kanda ya Afrika
- Details
Dayosisi yetu imepata heshima kubwa ya kushiriki katika Mkutano wa Kanda ya Afrika ulioandaliwa na United Evangelical Mission (UEM), uliofanyika katika mji wa Gaborone, nchini Botswana kuanzia tarehe 23 Februari hadi 1 Machi mwaka huu.
Katika mkutano huu muhimu dayosisi yetu imewakilishwa na viongozi na wajumbe wafuatao:
-
Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu
-
Mch. Happiness Diu – Mjumbe wa Bodi ya UEM Afrika anayewakilisha wanawake
-
Elvina Riziki – Mwakilishi kundi la vijana
- Hits: 2398
Askofu Dkt. Mbilu afungua Kikao Kazi cha Tathmini ya Mwaka 2025
- Details

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, amefungua rasmi kikao cha tathmini kwa kazi zilizotekelezwa katika kipindi cha mwaka 2025.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho kilichofanyika tarehe 12/02/2026 katika Hoteli ya Tumaini Mbuyukenda, Jijini Tanga, Askofu Dkt. Mbilu amesema kuwa lengo kuu la kikao hicho ni kuweka msingi imara kwa watumishi kutambua walipotoka, walipo na wanakoelekea katika utendaji wao wa kazi. Amesisitiza kuwa tathmini ni nyenzo muhimu katika kupima mafanikio, kubaini changamoto na kupanga mikakati madhubuti ya kuboresha utendaji kwa siku zijazo.
- Hits: 2818
Page 2 of 137

