ELCT North Eastern Diocese
Ufunguzi wa kikao cha tathmini ya kazi za Dayosisi kwa mwaka 2022.
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu leo tarehe 05/01/2023 amefungua kikao cha tathmini ya kazi za Dayosisi kwa mwaka 2022. Kikao kinafanyika katika hoteli ya Mbuyukenda Tanga.

- Hits: 12124
Waziri wa Nishati atembelea Makao Makuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki
- Details
Waziri wa Nishati, na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Mhe.January Makamba amefika katika Ofisi za Makao Makuu ya KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki leo tarehe 03/01/2023 na kutoa salamu zake za Mwaka Mpya, pongezi na shukrani kwa Askofu Dkt Msafiri Joseph Mbilu kwa ushirikiano mkubwa anaouonyesha katika ngazi ya jamii na Serikali kwa ujumla.
Mhe. January Makamba ameahidi kwamba wao kama viongozi wa Serikali wataendelea kutoa ushirikiano na kuunga mkono juhudi na mipango inayofanywa na KKKT-DKMs na Kanisa kwa ujumla ikiwemo kuona taasisi mpya ya KOTETI inainuka na kutimiza malengo makubwa mapya iliyopewa ya kuongeza ujuzi kwa watanzania kwa kozi ya ufamasia (Pharmacy) na kozi mbalimbali zitakazo endelea kutolewa katika Chuo hicho cha Kolowa Technical Training Institute (KOTETI) kinacho milikiwa na KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.
Kwa upande wake Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa mambo mengi ya maendeleo anayoyafanya sana sana mradi wa kufua Umeme wa Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere (JNHPP) ambao utasaidia katika upatikanaji wa umeme wa uhakika, kuondoa tatizo la uhaba wa umeme nchini pamoja na kupunguza gharama za umeme kwa Watanzania.
Askofu Dkt. Mbilu ameipongeza serikali kwa juhudi walizozionyesha kupitia Waziri wa nishati Mhe. January Makamba/ Mbuge wa Bumbuli kwa ushirikiano waliouonyesha na kuwashika mkono katika mchakato wa kuanzisha Chuo cha Kolowa Technical Training Institute (KOTETI.) ambacho kwa sasa tayari kinatoa Kozi ya Ufamasia (Pharmacy) inayohusika na kuandaa, kuchanganya na kutoa dawa za kimatibabu kwenye mahospitali, maduka ya madawa, na viwandani.

- Hits: 11844
Salamu za mwaka mpya 2023, za Baba Askofu Dkt. Msafiri Joseph Mbilu.
- Details
Askofu wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu, ametoa salamu za mwaka mpya wa 2023 kutoka kitabu cha Ayubu 22:21. “Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia.

Askofu Dkt. Mbilu akihubiri katika Ibada ya Jumapili na mwaka mpya 2023 leo tarehe 01/01/2023 katika Jimbo la Kusini Usharika wa Vuga ametoa wito kwa washarika na wakristo kwa ujumla kufungua mawazo nakumjua Mungu zaidi katika mwaka huu wa 2023 ili mema yaambatane nao. “Mungu tunaye paswa kumjua zaidi na zaidi uso wake hautatuacha”.

MKUU WA JIMBO LA KUSINI: MCH. ISSAI MWETA
Kwa upande wake, Mkuu wa Jimbo la Kusini Mch. Issai Mweta pamoja na kuwasihi wana KKKT-DKMs kuendelea kuiombea Dayosisi amewakumbusha wakristo wote kuombea amani ya nchi pamoja na kudumisha umoja.
- Hits: 11764
Salamu za Sikukuu ya Krismasi, 2022 KKKT-DKMs
- Details

“Isaya 9:2 “Watu wale waliokwenda katika giza wameona nuru kuu; Wale waliokaa katika nchi ya uvuli wa mauti, Nuru imewaangaza.”
- Hits: 12289
Page 63 of 137

