Uncategorised
- Details
Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania . Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) yenye Makao Makuu Wilayani Lushoto Mkoani Tanga ni miongoni mwa Dayosisi 28 za KKKT. Dayosisi inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) ni taasisi ya kidini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri za kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu wote. Taasisi hii KUPITIA COMPASSION INATANGAZA NAFASI MOJA YA MRATIBU WA HUDUMA YA MTOTO NA KIJANA (CHILD AND YOUTH DEVELOPMENT CENTER COORDINATOR (CYDC).
Utangulizi Mratibu wa Kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana ni mwajiriwa wa Kanisa na atatumika katika Kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana (KKKT – MKATA – TZ1211) kilichopo Sindeni – Wilaya ya Handeni.
1.1 MAJUKUMU
- Kuandaa Mpango wa mwaka wa Mshirika-Mwenza wa Kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana kwa kushirikiana na wadau wote na kuwasilisha kwa Kamati ya Huduma ya Mtoto kwa uthibitisho na kuidhinishwa na uongozi wa Kanisa.
- Kuwasilisha taarifa ya kimaandishi ya Utendaji na Maendeleo ya Kituo kwa amati, Uongozi wa Kanisa na Huduma ya Compassion International Tanzania kama itakavyo takiwa kwa pande zote husika.
- Kuhakikisha kuwa taarifa zote za fedha na Watoto zinatunzwa vizuri na kuhuishwa kila mara zinapohitajika.
- Kushiriki katika zoezi la Usaili wa kuwapata watendakazi wengine wote wa Kituo kwa kutoa maoni ya kitaalamu kuhusu nafasi hizo.
- Kuhakikisha mazingira ya walengwa kituoni ni salama kwao kujifunza na kushiriki katika programu zote za Kituo.
- Kuhamasisha upatikanaji wa Raslimali za ndani kwa ajili ya Miundombinu inayohitajika kwa walengwa kujifunza.
-
- Details
Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania . Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) yenye Makao Makuu Wilayani Lushoto Mkoani Tanga ni miongoni mwa Dayosisi 28 za KKKT. Dayosisi inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) ni taasisi ya kidini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri za kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu wote. Taasisi hii inatoa tangazo la kazi kwa nafasi moja ya MRATIBU WA HUDUMA YA MTOTO NA KIJANA kwa vijana wote (Wakristo)
NAFASI NA WAJIBU WA MRATIBU WA HUDUMA YA MTOTO NA KIJANA
- Details
Tarehe 19 Juni 1963, Kanisa la Usambara - Digo na makanisa mengine sita ya Kilutheri yaliungana na kuunda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania . Leo hii KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) yenye Makao Makuu Wilayani Lushoto Mkoani Tanga ni miongoni mwa Dayosisi 28 za KKKT. Dayosisi inaitwa hivyo kwakuwa inapatikana Kaskazini Mashariki mwa Tanzania katika Mkoa wa Tanga. Kwahiyo KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (KKKT-DKMs) ni taasisi ya kidini iliyosajiliwa tarehe 19 Juni 1963 na Makao yake Makuu yapo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga. Dhamira ya KKKT-DKMs ni kufundisha na kuhubiri neno la Mungu na kutoa huduma nzuri za kiroho, kimwili, kiakili, kiuchumi na kijamii kwa watu wote. Taasisi hii KUPITIA COMPASSION inatangaza nafasi moja ya kazi ya Mtendakazi wa Huduma ya Kunusuru Maisha ya Mama na Mtoto.
SIFA ZA MTENDAKAZI WA HUDUMA YA KUNUSURU MAISHA YA MAMA NA MTOTO
NAFASI: Mtenda kazi katika Huduma ya Kunusuru Maisha ya mama na mtoto (HBI).
MAHALI: Kituo cha huduma ya mtoto na kijana.
KUWAJIIBIKA: Atawajibika kwa Mratibu wa kituo cha huduma ya maendeleo ya mtoto na kijana.
Muhtasari wa majukumu ya kazi kwa mtendakazi
Mtendakazi wa huduma ya afua ya kunusuru maisha ya mama na mtoto kwa huduma za nyumbani (Survival & Sponsorship Home Based) atahusika moja kwa moja na akina mama na watoto watakaonufaika na huduma hii. Atatumia asilimia 80% ya muda wake wa kazi kwa kuwatembelea akina mama hao nyumbani kwao na kutoa mafunzo kwa kutumia mitaala mbalimbali ya afua hii. Yeye ndiye atawajibika kutekeleza afua akishirikiana na watendakazi wengine katika kuhakikisha masuala yote katika program ya afua ya mama na mtoto yanatekelezwa. Ni jukumu la mtendakazi kufuatilia mwenendo wa namna malengo ya afua ya mama na mtoto yatakavyosababisha tofauti kwa walengwa katika maisha ya kila siku Mtendakazi atafuatilia na kuhakikisha upimaji wa ukuaji wa mtoto unafanyika kila mwezi kwa utaratibu uliowekwa na kuingiza taarifa kwenye mfumo wa mawasiliano wa Connect. Awe ni mfano wa kuigwa katika ukristo wake, anayeheshimu watu na mwenye kutunza siri za watu.
Page 1 of 119