
Askofu Mteule Mch. Dr. Msafiri Mbilu na viongozi wengine wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki pamoja na uongozi wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa SEKOMU wamemtembelea Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa .

Ambapo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameutaka uongozi mpya wa KKKT-Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ambao ndio wamiliki wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa (SEKOMU) ukamilishe mahitaji ambayo yataiwezesha Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kukiruhusu chuo hicho kuendelea na udahili.
Mhe. Kassim Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Jumamosi, Januari 16, 2021 wakati alipokutana na Askofu Mteule Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ambaye aliambatana na viongozi wengine wa Dayosisi. Kikao kimefanyika katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa Dododoma.

Dean Mteule wa KKKT-DKMS,Mch. Michael Kanju akisalimiana na WAZIRI MKUU waTanzania,Mhe.Kassim Majaliwa

Kaimu Katibu Mkuu wa KKKT-DKMS Mch. Godfrey Walalaze akisalimiana na WAZIRI MKUU waTanzania, Mhe.Kassim Majaliwa

Mkuu wa Jimbo Mteule wa jimbo la Pwani Mch. Thadeus Ketto akisalimiana na WAZIRI MKUU waTanzania, Mhe.Kassim Majaliwa

Mkuu wa Jimbo Mteule wa jimbo la Kaskazini Mch.Anderson Kipande, akisalimiana na WAZIRI MKUU waTanzania,Mhe. Kassim Majaliwa

Mkuu wa Jimbo Mteule wa jimbo la Tambarare Mch. Frank Mtangi, akisalimiana na WAZIRI MKUU waTanzania, Mhe. Kassim Majaliwa

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha SEKOMU Prof. Vincent Kihiyo, akisalimiana na WAZIRI MKUU wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Mipango,Fedha na Utawala Prof. Joseph Mbatia akisalimiana na WAZIRI MKUU wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa
Mhe. Kassim Majaliwa, ametumia fulsa hiyo kuwashukuru viongozi wa Dini Nchini kwa mchango mkubwa kwa Taifa ambapo amesema "Viongozi wa Dini ni watu muhimu sana, Inchi imetulia na ina amani , hivyo kuwa kimbilio kwa waliokosa amani makwao"

