ELCT North Eastern Diocese
Mwendelezo wa ziara ya Askofu Dkt. Mbilu kutembelea Jimbo la Pwani na Sharika
- Details
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch Dkt. Msafiri Joseph Mbilu ameendelea na ziara yake ya kutembelea Jimbo la Pwani na Sharika zake ambapo tarehe 20/04/2024 ametembelea Usharika Mteule wa Lugongo na kuongoza Ibada ya Shukrani.
- Hits: 193
Tamati ziara ya Askofu Dkt. Mbilu Jimbo la Pwani
- Details
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Mch.Dkt. Msafiri Joseph Mbilu amehitimisha ziara yake ya siku tatu ya kutembelea Jimbo la Pwani na Sharika zake kwa kuongoza Ibada ya Jumapili katika Usharika wa Maramba katika Jimbo la Pwani.
- Hits: 203
Askofu Henrik Stubkjæ atoa wito kupima Afya mara kwa mara
- Details
Rais wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF) Askofu Henrik Stubkjær ameungana na Watanzania katika kuadhimisha siku ya ugonjwa wa Hemophilia Duniani ambapo jamii imeaswa kupima mara kwa mara ili kuweza kujua hali ya Afya zao na kuchukua hatua mapema.
- Hits: 512
Askofu wa KKKT aahidi kuendeleza ushirikiano na LWF
- Details
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Askofu Dkt. Alex Malasusa amesema kuwa ujio wa Rais wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (LWF), nchini Tanzania Askofu Henrik Stubkjær utaendelea kuimarisha uhusiano uliopo na Makanisa ya Kilutheri duniani katika kulitangaza neno la Mungu.
- Hits: 607
Page 1 of 107